Bilionea nchini Tanzania, Mohamed Dewji 'Mo' Amepatikana Akiwa Hai Leo

Kwa ufupi
Bilionea nchini Tanzania, Mohamed Dewji 'Mo' amezungumza kwa mara ya kwanza baada ya kupatikana akiwa hai

Mo alimepatikana alfajiri ya leo Jumamosi Oktoba 20, 2018

'Mo' Dewji: Namshukuru Mungu
Mohammed Dewji 'Mo'
Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania

Mohammed Dewji 'Mo' anamshukuru Mungu kwa kumrejesha salama.
Mo aliyepatikana alfajiri ya leo Jumamosi Oktoba 20, 2018 amesema hayo kupitia akaunti ya Twitter ya Kampuni ya Mohamed Enterprise Limited (Metl Group).
"Namshukuru mwenyezi Mungu nimerudi salama nyumbani. Nawashukuru Watanzania wenzangu na watu wote kote duniani kwa dua na sala zao."
"Nashukuru mamlaka zote, ikiwemo jeshi la polisi, zilizofanya kazi ya kuhakikisha narudi salama," amesema Mo

Mo amepatikana ikiwa ni siku ya tisa tangu alipotekwa na watu wasiojulikana alfajiri ya Oktoba 11,2018 katika Hoteli ya Collosium jijini Dar es Salaam alikokuwa amekwenda kufanya mazoezi.

No comments:

Post a Comment

Active Visitors

Pages