MAMBO MUHIMU YAKUZINGATIA KABLA HUJAANZA UFUGAJI


Halowww habar rafiki
  Natumai wote hamjambo ,leo ninapenda kushare nanyi somo linalohusu ufugaji wa kuku wa Kienyeji na Chotara
 Kuna mambo muhimu ya kuzingatia kabla hujaanza kufuga nayo ni

1)Soko:Kitu cha kwanza kabisa unachotakiwa kuangalia ni soko la muda huo linataka nn kama ni kuku wawe kuku aina gan au mayai yap yanatakiwa hii itakusaidia ww kuingia kwenye soko la
2)Mtaji : Ni vizur uangalie una mtaji kias gan ili ujue utaanza vip biashara yako kama itakuwa ya mtaji mkubwa au mdogo,na hata kama una mtaji mdogo usiogope ,unaweza ukaanza na mtaji mdogo ukaukuza hadi ukakua
 Unaweza ukaanza hata na kuku 10,ukawazalisha wakawa wengi

3)Banda bora :lazima uwe na banda bora kwa ajili ya kufugia kuku wako
 Na kuna aina mbili za mabanda
   Mabanda ya ghorofa
    Mabanda ya kawaida
Sifa za banda bora
Lijengwe kwa kuzingatia hali ya hewa ya eneo husika pamoja na uelekeo wa upepo
Ukubwa wa banda uendane na idadi ya kuku
Banda lisiwe linahifadhi uchafu
Unaweza ukaweka wavu juu ya banda ili kuku wakae juu na wakinya kinyesi kidondoke chin
Unaweza ukajaza maranda kwa kimo cha nchi 3-3
 Liwe na vyombo vya maji na chakula vya kutosha
  Lisiwe linavuja wala kupitisha upepo
   Liwe na mlango na madirisha makubwa
 
Liwe linatenganisha kuku kulingana na umri wao
 Liwe na viota kwa ajili ya kutagia na kuatamia mayai

4)Lishe bora:Ili upate matokeo mazur kwenye ufugaji wako laxima uwape kuku wako lishe bora

5)Mbegu bora:Matumizi ya mbegu bora yamekuwa ni changamoto kubwa kwa wafugaji walio wengi wa kuku hapa unatakiwa uwe makini sana wakat wa kuchagua mbegu za kuku
     Baadhi ya mbegu bora za kuku

       Kuchi
        Shilole-kishingo
        Singamaganzi nk

6)Malezi bora na tiba:Walee kuku wako vizuri na uwape chanjo na tiba kwa wakati kila uonanapo dalili za ugonjwa

  Kuna aina kuu tatu za ufugaji
     Ufugaji wa ndani ya mabanda
     Ufugaji wa nusu ndan nusu nje
     Ufugaji huria

No comments:

Post a Comment

Active Visitors

Pages